• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

DC SHINYANGA AONYA SIASA ZA MAJITAKA MWAMAGUNGULI

Posted on: June 21st, 2017

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amewaonya wananchi wa kijiji cha Mwangunguli kata ya Kolandoto katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kuacha tabia ya kuwasikiliza viongozi wa siasa ambao wanahujumu juhudi za Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo. Mheshimiwa Josephine Matiro ameyazungumza hayo katika kijiji hicho alipoenda kuwasikiliza maoni ya wananchi ikiwa ni mojawapo ya kituo maalumu kati ya vituo mbalimbali  vilivyotengwa kusikiliza maoni ya wananchi katika juma zima la Utumishi wa Umma.

Mmoja wa wananchi Shija Luhende akieleza mbele ya mkuu wilaya kuwa maji hayafai- (Picha kwa hisani ya Marco Maduhu na Malunde Blog)

Baada ya kufika katika kijiji hicho akiwa ameambatana na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya hiyo pamoja na viongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga akiwemo Mkurugenzi wa Manispaa, walizungumza na wananchi wa eneo hilo ambapo hoja ya mgogoro wa mradi wa maji ya kisima kirefu katika kijiji hicho ilisikilizwa.Ilielezwa kuwa mradi huo wa maji ambao ujenzi wake ulikamilika mwaka 2014 kwa gharama ya shilingi 294.6 ulikuwa haujatumika kuhudumia wananchi kutokana na propaganda zilizokuwa zikienenezwa na viongozi wa kuanzia ngazi ya kitongoji hadi kata wakidai kuwa maji ya kisima hicho yana chumvi na hata yakitumika kupikia chakula yanakibadilisha na kuwa na rangi ya njano.

Mkuu wa wilaya Josephine Matiro akinywa maji yaliyoaminika kuwa hayafai kwa matumizi ya binadamu-(Picha kwa hisani ya Marco Maduhu na Malunde Blog)

Kufuatia utata huo Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Manispaa Geoffrey Ramadhan Mwangulumbi na baadhi ya wananchi waliamua kunywa maji na kuagiza chakula kipikwe kwa kutumia maji hayo ili wathibitishe kama maji hayo yana chumvi pia kama yanabadilisha chakula kuwa cha njano. Mara baada ya kunywa maji hayo, mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi na wananchi wote walithibitisha kuwa maji hayo hayana chumvi na yanafaa kwa matumizi ya binadamu.

Na mara baada ya chakula ‘wali’ kupikwa katika nyumba iliyokuwa jirani na eneo la mkutano, kililetwa mbele ya mkutano na kuwaonyesha wananchi rangi ya chakula inayoonekana baada ya kupikwa kwa kutumia maji ambayo yalitangazwa na viongozi wao kuwa yanabadilisha rangi ya chakula. Chakula kilicholetwa kilikuwa na rangi nyeupe kama ilivyo kawaida ya rangi ya chakula hicho, hali ambayo ilisababisha minong’ono miongoni mwa wananchi na baadhi ya viongozi wao wa kisiasa kuanza kuondoka wakiwa na aibu tele.

Baada ya kunywa maji na kuona chakula hakijabadilika rangi, mkuu wa Wilaya alisema kuwa amegundua kuwa viongozi wa kijiji hicho ambao ni wanasiasa wamewasababishia wananchi wao shida wakiwemo akina mama na watoto kutembea umbali mrefu wakitafuta maji na kuacha maji yaliyo karibu na makazi yao. Mara baada ya kutatua mgogoro huo, mkuu wa Wilaya aliukabidhi mradi huo kwa wananchi wa kijiji wakishirikiana na wataalam  wa Manispaa.

Mkurugenzi wa Manispaa akionesha chombo kitupu mara baada ya kunywa maji ambayo yaliyokuwa yakipotoshwa na vingozi wa siasa kuwa hayafai kwa matumizi ya binadamu.(Picha kwa hisani ya Marco Maduhu na Malunde Blog)

Mwananchi wa Kijiji cha Mwamagunguli akinywa maji ya maradi uliokuwa na mgogoro kuwa maji yake yana chumvi na yanabadilisha rangi ya chakula.(Picha kwa hisani ya Marco Maduhu na Malunde Blog)


Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga