• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MJEMA AKABIDHI MKOPO WA ZAIDI YA MILIONI 100, ASISITIZA UZINGATIAJI WA SHERIA

Posted on: December 2nd, 2022

Na George Mganga, Shinyanga Manispaa

MKUU wa Mkoa wa Shinyanga, Mh. Sophia Mjema, amevitaka vikundi vilivyopata mkopo wa Pikipiki kutumia vyombo vya usafiri kwa kuzingatia sheria za usalama bararabani.

Rai hiyo ameitoa leo Disemba 2, 2022, wakati wa ukabidhishaji mikopo kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwenda kwa vikundi tisa (9) yenye thamani ya Tshs. Milioni mia moja arobaini na nne, laki nne na elfu ishirini nan ne (144,424,00).

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mh. Sophia Mjema, akizungumza katika hafla ya ukabidhishaji mikopo kwa makundi 9.

Akikabidhi mikopo hiyo iliyotolewa na Manispaa kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa kipindi cha robo ya pili ya 2022/2023, Mjema amesisitiza utii wa sheria bila shuruti, akieleza ndiyo kinga kuu ya usalama barabarani.

“Mmepata pikipiki hizi nzuri, sasa ni wakati wa kwenda kuzitendea haki huko kwa kuzingatia sheria zilizowekwa. Naomba zisiende kutumika katika uhalifu bali kazi iliyokusudiwa.

“Muache kupakiza mizigo ambayo haiendani na pikipiki, tunaona wengine wamekuwa wakipakiza mbao ambazo zinachukua nafasi kubwa ya barabara, hili halitakiwi, kuna magari maalum ya kubeba hizo mbao, na mtakaokiuka maagizo, hatua za kisheria zitachukuliwa”, amesema Mjema.

Kwa upande mwingine, Mh. Mjema amewaasa wanavikundi wote waliopewa mikopo, waende kuitumia kwa makusudio ya miradi pekee na si vitu vingine ili waweze kurejesha, huku akitoa msisitizo wa kufanya marejesho haraka na kwa wakati mwafaka.

Wanakikundi waliopewa mkopo wa Pikipiki katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mh. Jasinta Mboneko.

Wakati huo, Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Mh. Jasinta Mboneko ameeleza kuwa watashiriki kikamilifu kusimamia zoezi la urejeshaji wa mikopo iliyotolewa na Manispaa ili kuwasaidia wengine pia kukopeshwa sambamba na kutoa elimu ya usalama barabarani kwa waendesha pikipiki.

“Tutaendelea kutoa elimu ya usalama barabarani ili kuepusha ajali ambazo zinapunguza nguvu kazi ya taifa, mbali na hilo pia tutahakikisha mikopo yote iliyokopeshwa inarejeshwa kwa wakati ili kusaidia wengine." amesema Mboneko.

Naye Mh. Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Elias Masumbuko, ameongeza kwa kusema kuwa Vijana, Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu wengine wanaohitaji mikopo wanakaribishwa kuomba mkopo, kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa ili kuongeza nguvu kazi ya taifa.

Mh. Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Elias Masumbuko, akizungumza katika hafla hiyo.

Masumbuko amebainisha hayo akieleza kuwa lengo la Manispaa ni kukuza ustawi wa maendeleo kwa makundi yote kujiongezea kipato.

Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga, John Tesha, amevitaja vikundi vilivyopatiwa mkopo kuwa ni YOSE, Marida, Hisa Mageuzi, Princess, Ushonaji B (Wanawake), Nguvu Kazi, Waendesha Bodaboda Kata ya Mjini, Waendesha Bodaboda Bushola na Kikundi cha Wezesha Maisha kutoka kata ya Chamaguha.

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga