• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe |
    • Malalamiko |
Shinyanga Municipal Council
Shinyanga Municipal Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Rasilimali Watu
      • Elimu ya Sekondari
      • Elimu ya Msingi
      • Fedha
      • Ujenzi
      • Kilimo na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Mipango, Ufuatiliaji na Takwimu
      • Hearth
      • Usafi na Mazingira
      • Land and Natural Resources
    • Vitengo
      • Tecknolojia, Habari, Mawasiliano na Uhusiano
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Usimamizi wa Ununuzi
      • Nyuki na Maliasili
  • Fursa za Uwekezaji
    • Uwekezaji wa Viwanda
    • Fursa za kilimo
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Fursa za elimu
    • Fursa za Afya
  • Huduma Zetu
    • Huduma ya Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma ya kilimo
    • Huduma za Ufugaji
    • Ufugaji wa Samaki
    • Huduma za Watumishi
    • Huduma ya utoaji wa Mikopo
    • Kukondisha Vyumba vya Biashara
    • Unyonyaji wa Maji Taka
    • Huduma za Biashara
      • Leseni za Biashara
      • Elimu ya kibiashara
      • Ukaguzi wa Viwanda
      • Usimamizi wa Masoko
      • Prepalation of Good Environment for Investment
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha na Utawala
      • Kamati ya Uchumi, Afya na Elimu
      • Kamati ya Miundombinu
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba ya kamati za Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iIliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo za Halmashauri
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za maombi
    • Miongozo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Mafunzo

MSTAHIKI MEYA WA MANISPAA YA SHINYANGA DAVID NKULILA AFARIKI DUNIA.

Posted on: August 23rd, 2021

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga David Mathew Nkulila (57) ambaye ni Diwani kata ya Ndembezi kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumatatu Agosti 23,2021 wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga kutokana na maradhi yaliyokuwa yanamsumbua.


Nkulila amekuwa Diwani wa kata ya Ndembezi tangu mwaka 2010 na Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mwaka 2010-2015.


Nkulila alichaguliwa kuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Novemba 24 Mwaka 2020 na ametumikia nafasi ya Meya kwa kipindi cha miezi 10 hadi umauti ulipomkuta.


David Mathew Nkulila alikuwa na maono ya kuifanya Manispaa ya Shinyanga kuwa Jiji.


 Nkulila atakumbukwa kwa misimamo yake thabiti katika kutetea wanyonge, asiyekubali kuyumbishwa na kupiga vita rushwa na ufisadi. 


Msiba upo nyumbani kwake mtaa wa Mabambasi kata ya Ndembezi jirani na Kanisa la Moravian, taratibu za ratiba za mazishi tutawataarifu.



Historia fupi ya Marehemu David Nkulila 


David Mathew Nkulila alizaliwa tarehe 16/04/1964, Tabora mjini, mkoa wa Tabora.


David Mathew Nkulila alianza darasa la kwanza katika shule ya Msingi Bunda mwaka 1974, na baadae Shule ya Msingi Mkendo mwaka 1975, alihamia Shule ya Msingi Old Shinyanga mwaka 1976 na baadaye Shule ya Msingi Mwenge-Shinyanga  mwaka 1977 hadi alipohitimu darasa la saba mwaka 1980 katika shule hiyo.


Baba yake mzazi na Marehemu Nkulila alikuwa mtumishi wa serikali hali iliyopelekea Marehemu Nkulila kuhama Shule moja kwenda nyingine ili kumfuata baba yake sehemu alipohamishiwa.


Marehemu David Mathew Nkulila alipata elimu yake ya Sekondari katika Shule ya Sekondari ya Kilimo Kilosa (Kilosa Agricultural Secondary School) kati ya mwaka 1981-1984. Shule hii ya Sekondari ya Kilimo Kilosa ni maarufu hapa nchini kwa kauli mbiu yake ya "Elimu na Kazi"


Baada ya kuhitimu kidato cha nne Marehemu Nkulila alijiajiri na kazi ya Kilimo ambayo ndiyo ilikuwa kazi yake ya msingi hadi mauti yalipomkuta leo 23/08/2021.


Historia yake ndani ya Chama Cha Mapinduzi na majukumu ya kisiasa


Marehemu David Mathew Nkulila ana uzoefu wa kutosha katika masuala ya siasa. Marehemu Nkulila alijiunga na Chama Cha Mapinduzi(CCM) mwaka 1995. Ndani ya CCM Marehemu Nkulila amewahi kushika nyadhifa mbalimbali.


⏩ Marehemu Nkulila amewahi kuwa mjumbe wa Kamati ya Siasa ya wilaya ya Shinyanga Mjini kati ya mwaka 2013-2017


⏩ Katibu wa CCM Kata ya Ndembezi kati ya mwaka 2007-2012.


⏩ Katibu wa CCM Kata ya Ngokolo.


⏩ Katibu wa CCM Tawi la Bugoyi kati ya mwaka 2003-2007.


Nafasi alizozitumikia


⏩ Marehemu Nkulila amekuwa Diwani wa Kata ya Ndembezi kwa vipindi vitatu mfululizo toka mwaka 2010 hadi leo tarehe 23/08/2021 mauti yalipomkuta.


⏩ Marehemu Nkulila amekuwa Naibu Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kati ya mwaka 2013-2015.


⏩  Marehemu Nkulila amekuwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Mabambasi kati ya 2004 - 2019.


⏩ 2000-2003 Mwenyekiti wa kamati ya WES mtaa wa Mabambasi.


⏩  Amekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Shinyanga (SPC) kwa zaidi ya miaka 10.


Kazi alizozifanya akiwa Diwani wa Kata ya Ndembezi


Marehemu David Mathew Nkulila kwa kipindi chake chote akiwa kama diwani wa Kata ya Ndembezi alifanikiwa kuwawakilisha vema kwa uadilifu mkubwa wakazi wa Kata ya Ndembezi.


(a)Alisimamia upimaji wa ardhi (viwanja) katika Mitaa ya Ndembezi na Butengwa. Awali mitaa hii ilikuwa na hadhi ya vijiji na ardhi ilikuwa haijapimwa.


(b) Alisimamia ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya barabara katika viwango vya lami na changarawe ikiwemo mitaro, makalvati, vivuko na madaraja.


(c) Alisimamia ujenzi wa machinjio ya kisasa yaliyopo katika mtaa wa Butengwa.


(d)Alisimamia ujenzi wa Zahanati ya Kata ya Ndembezi iliyopo katika mtaa wa Butengwa. Kwa sasa ujenzi huo upo katika hatua ya boma. Eneo hili la ujenzi wa Zahanati lilipatikana kufuatia juhudi zake akishirikiana na ofisi ya Mtendaji wa kata ya Ndembezi.


(e) Alisimamia utolewaji wa mikopo ya bila riba inayotolewa na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kutoka 10% ya mapato yake ya ndani kwa makundi ya vijana, wanawake na walemavu.


Mambo aliyoyapenda (Hobby)


Marehemu Nkulila alipenda kusoma vitabu, majarida na magazeti, Mitandao ya Kijamii na alipenda sana kuendesha baiskeli.

R.I.P Mstahiki Meya Nkulila

Tangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MADEREVA April 14, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA April 27, 2023
  • MAADHIMISHO YA WIKI YA UNYONYESHAJI WA MAZIWA DUNIANI August 04, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAONESHO YA NANENANE 2023 July 31, 2023
  • Tazama

Habari Mpya

  • ALAT YAIPONGEZA MANISPAA YA SHINYANGA KWA UTEKELEZAJI MZURI UJENZI WA JENGO LA UTAWALA.

    May 08, 2025
  • MHE.MASUMBUKO AWATAKA MADIWANI KUSHIRIKIANA KIKAMILIFU KUKABILIANA NA WIZI WA VIFAA VYA MIRADI YA MAENDELEO.

    May 07, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI MANISPAA YA SHINYANGA LAMPONGEZA MKURUGENZI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA MAAGIZO

    May 06, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUBORESHA SHULE YA WASICHANA SHINYANGA ILI KUIFANYA KUWA MIONGONI MWA SHULE BORA NCHINI “. NDG. MSIGWA.

    May 03, 2025
  • Tazama

Video

MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA MANISPAA YA SHINYANGA 2024
Video Zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • Tangazo la nafasi ya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga
  • Urban Sanitation and Hygiene | Mazingira Safi Maisha Bora
  • Ripoti mbalimbali
  • Sheria Ndogondogo za Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Tovuti Nyingine tunazohusiana

  • Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa(TAMISEM)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknologia
  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Mkoa wa Shinyanga
  • Sekretarieti ya Ajira

wasomaji mbalimbali duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya eneo

Wasiliana Nasi

    Tanesco S, Mwanza Road

    Anwani ya Posta: P.O.Box 28 Shinyanga

    Simu: +255-28-2763213

    Simu ya Mkononi: 0759 023 788

    Baruapepe: md@shinyangamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Ramani ya Tovuti
    • Sera ya faragha
    • Kanusho

Haki zote zimehifadhiwa@2018.Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga